DJ CHOKA afungua fulsa kwenu wanawake WATATU MNAOJUA KUCHANA! (SOMA hapa)

Habari zetu wadau,
Natumaini kila mtu yuko poa, sasa waswahili husema biashara asubuhi jioni mahesabu sasa ikiwa mwaka ndio kwanza bado unanukia upya nimeona niwape habari hii. Natafuta wasichana au wadada 3 ambao wanajua kurap au kuchana kwa vijana wanavyosema kwa uzuri kabisa na kunata na beat. Wasicha hao wawe kwanza na mwonekano wa kisanii na wawe na kipaji kweli chakuchana FREE STYLE. Shindano hilo litaanza tarehe 14.1.14 hadi tarehe 24.1.14
Ili kushiriki shindano hilo kwanza unatakiwa uwe mtumiaji wa Instagram ambapo utatakiwa kufollow account ya @chokadj www.instagram.com/chokadj halafu utajirecord video itakayokuwa inakuonyesha kufreestyle kitu chochote kwa lugha ya Kiswahili na English kwa second 16 na kisha utaweka hash tag hii #ChokaNaFreeStyle2014 halafu utaituma kwenye account yako ya Instagram, mdada atakayepata LIKE nyingi kwenye hiyo clip ndio atakuwa ananafasi kubwa yakushinda.
Shindano hili ni kwa wadada wanaoishi DAR ES SALAAM Pekee, washindi hao watatu wataingia katika mixtape yangu na watarekodi wimbo wao wa pamoja pale B’HITZ STUDIO na pia watafanyiwa video ya wimbo huo na pia watapata PROMO ya kazi zao kupiti website hii ya DJCHOKA MUSIC.

Comments

CONVERSATION

0 comments :

Post a Comment

Back
to top